Unknown



 Imeandaliwa na
 Charles Stephen Asande
Leo nataka tujifunze kuhusu mteja.Hapa tutapata kujua mambo tofauti tofauti yamhusuyo mteja.
 Makampuni yaliyoendelea yana fokasi kwa mteja,Yanajipanga kufikia mahitaji ya wateja.

Mteja ni nani?
    -Mteja ni mtu anayehitaji huduma/bidhaa/msaada kutoka kwako
-Mteja ni sababu ya wewe kuwa hapo ulipo.


-Mawasiliano baina ya mtoa huduma na mteja
Huduma nzuri kwa mteja ni ile ya kummsaidia mteja zaidi ya kile anachouliza.

MBINU BORA KUMVUTA WATEJA

-Vaa vizuri
-Furahia kusaidia watu
-Wahudumie vizuri
-Wajali wateja wako
-Wahudumie kwa usawa
-Tambua watu wenye mahitaji ya pekee
-Kuwa msafi
-Jiamini
-Kuwa na mpangilio mzuri

WATEJA WENYE MAHITAJI YA KIPEKEE

-Wateja wanaozungumza lugha tofauti
-Watu wenye ulemavu
-Wageni wa mji au maeneo ulipo
-Watoto

JINSI YA KUMHUDUMIA WATEJA

-Kuwa shapu,msalimu na kumkaribisha mteja mara moja unapomuona hata kama upo bize
-Tabasamu
-Usitumie lugha ya ukali
-Mwache awe huru
-Muulize anachohitaji usihisi ni nini anaweza hitaji
-Mfanye ajione ni muhimu kwako na unamthamini
-
-Msikilize kwa umakini
-Tambua tamaduni za watu wa mazingira(ili uweze wasalimia na kuwakaribisha ipasavyo)
-Mtambulishe aina,ubora wa bidhaa na huduma yako.
-Maliza kwa kuwashukuru na kumkaribisha tena
-Waelimishe  wateja wako.
Kumbuka:-Huduma kwa mteja inaisha pale anaporidhika.
        -Wewe sio mteja! hivo sio kila unachokiona ni ubora katika bidhaa na mteja atakiona hivohivo(msikilize )

MAMBO YA KUEPUKA KUFANYA KWA MTEJA

-Kumwambia Sijui bila kumpa mbadala
-Kutokumjali mteja kwa kuwa upo bize
-Kuwahudumia kwa utofauti(kujali baadhi na kutojali wengine)
-Kumtolea lugha chafu



like our facebook page  Vijana Tunaweza Kujiajiri



0 Responses

Chapisha Maoni